Baba Mtakatifu Francisko hana mpango wa kuwatoa wagonjwa mapepo, kama walivyodai baadhi
ya waandishi wa habari kwa siku za hivi karibuni, walipomwona Baba Mtakatifu akimwekea
mgonjwa mikono juu ya kichwa chake alama ya kumwombea. Ni ufafanuzi unaotolewa na
Padre Federico Lombardi msemaji mkuu wa Vatican.
Baba Mtakatifu anapokutana
na wagonjwa anawaombea na kusali pamoja nao na kwamba, kitendo cha Baba Mtakatifu
Francisko kumwekea mgonjwa mikono kichwani haikuwa ni alama ya kutaka kumtoa mapepo
au kumfanyia miuujiza.