2013-05-21 10:05:26

Mfanyabiashara apanda juu ya Kinara cha Kanisa kuu la Mtakatifu Petro ili kuwashutumu wanasiasa!


Bwana Marcello Di Fenizio,mfanyabiashara kutoka Italia, siku ya jumatatu alipanda kwenye Kinara cha Kanisa kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican, akipinga vitendo vya wanasiasa wa Italia ambavyo vimepelekea hali ngumu ya uchumi pamoja na kutoweka kwa fursa za ajira nchini Italia. Bwana Fenizio alitandaza bango lake akimwomba Baba Mtakatifu Francisko kuingilia kati ili kuokoa "Jahazi" la watu wanaokata tamaa.

Akizungumzia tukio hili, Padre Federico Lombardi, msemaji mkuu wa Vatican anabainisha kwamba, Bwana Fenizio hana jipya, kwani hii si mara ya kwanza kupanda kwenye Kinara cha Kanisa kuu la Mtakatifu Petro kwa madai dhidi ya wanasiasa. Amekwisha wahi kufanya hivyo dhidi ya Serikali ya Professa Mario Monti. Madai yake ya sasa anayaelekeza dhidi ya Jumuiya ya Ulaya.







All the contents on this site are copyrighted ©.