2013-05-20 14:51:24

Papa azindua katika Smartphone-habari za Fides


Shirika la habari za kimissionari la Fides, limetangaza kwamba, habari zake zitapatikana katika lugha nane, kupitia mpango wa smartphones, unayoitwa "Missio", ambao unaopatikana bil malipo yaani bure.
Huduma hii ilizinduliwa na Papa Fransisko wakati alipokutana na Wakurugenzi wa Mashirika ya Kipapa ya Kitume ya Kitaifa ya Missioni na pamoja na wafanyakazi wa Fides, Ijumaa iliyopita , Mei 17 mjini Vatican.
Papa Francesco ilizindua utoaji wa habari huo kwa kubofya juu ya iPad, kama alivyombwa na Padre Andrew Small, OMI, Mkurugenzi wa Kitaifa wa Mashirika ya Mashirika ya Kipapa ya Misioni nchini Marekani.
Ukurasa huu wa Utume wa uinjilishaji , utakuwa unatoa habari za Kanisa zilizotolewa kupitia tovuto ya habari za Vatican "news.va", pia kuna picha, sinema na homilia za Papa, habari ya Kanisa katika ulimwengu na zitakuwa zikitolewa katika lugha nane.
Padre Small katika uzinduzi huo alimwambia Baba Mtakatifu,kwamba wanalenga kuiweka Injili, ndani ya mfuko wa kila kijana ulimwenguni ,maneno yaliyomgusa Papa Fransisko wakati akibofya kifungo kilichoandikwa juu yake maneno “sisi ni wainjilishaji”.
Katika siku yake ya kwanza ya kuzinduliwa kwa ukurasa huu, jumla ya watu 1,140 wa kutoka nchi 27 tofauti, waliutembelea ukurasa huo. Padre Small anasema lengo letu ni kuwasaidia watu kuiona dunia kupitia macho ya imani". Ukurasa huu unapatikana katika iTunes App na Google Play , ambamo ujumbe wa uinjlishaji, unatolewa katika lugha nane: Kiingereza, Kihispania, Kiitaliano, Kijerumani, Kifaransa, Kireno, Kichina na Kiarabu.Karibuni nyote.







All the contents on this site are copyrighted ©.