2013-05-20 15:12:06

Kwa maji ya ubatizo mnakuwa mwendelezo wa Ukristu nyakati zote ...


Jumapili, katika kukamilisha maadhimisho ya Siku Kuu ya Pentekoste, Rais wa Baraza la Kipapa kwa ajili ya kukuza Uinjilishaji Mpya, Askofu Mkuu Rino Fischella, alitoa hotuba fupi ya shukurani kwa niaba ya wanaharakati wote wa Kanisa, vyama vya walei na jumuiya za kikanisa, ambamo alitaja katika kipindi hiki za siku hizi mbili,Jumamosi na Jumapili, wameziishi hisia halisi za nguvu mpya iliyotoka juu, kama Bwana Yesu alivyo ahidi wanafunzi wake.
Hivyo wanaharakati kutoka jumuia na vikundi mbalimbali waliojumuika katika mkusanyiko huu, wao pia kwa maji ya ubatizo, wote wanakuwa ni mwendelezo wa daima wa imani ya nyakati zote, na katika kuyatolea sadaka maisha katika utendaji wa kila siku kwa nguvu ya zawadi yake Roho Mtakatifu. Nguvu hii ni uwezo wa kubadilisha moyo, kubadili namna za kufikiri na kutenda, na kufanya hivyo, ni uwezo wa kupenda. Kuwa na upendo unaokwenda zaidi ya upeo wetu wenyewe kwa sababu unatokana kwa Kristo Mfufuka, na kuiingia upya moyoni kama matunda ya Roho Mtakatifu, mwenye kuongoza katika maisha ya ubinadamu wote kwenye mipaka yake ya kidunia.

Askofu Mkuu Fisichella , alimshukuru Papa kwa hotuba yake aliyoitoa wakati wa mkesha wa Pentekoste, ambamo kwa shauku kubwa ya kiinjili, alionyesha njia ya kutenda zaidi , kwa ajili ya kupata matunda zaidi, katika utume wa walei na jumuia za kikanisa mbalimbali, duniani.
Na aliirejea hotuba ya Papa, ambamo aliwakumbusha daima kumweka Kristo kuwa kituo kikuu cha rejea, kwa sababu, ni kwa namna hiyo tu Kanisa hubaki kuwa lenyewe, bila ya kufungwa na nguvu za hofu na mashaka. Na kwamba, utume wa kuinjilisha kwa ujasiri na uvumilivu, kinyume chake ni lazima kushinikiza ujenzi wa utamaduni wa kukutana, kuruhusu kuona na kugusa mwili wa Kristo. Kweli, katika Ekaristi Takatifu Bwana Mfufuka, huwafanya wote kuwa na nguvu mpya ya kurudi katika jumuiya, ambamo kila mmoja huiishi imani yake.
Kwa nguvu za Mwili wa Kristu chakula chetu, tunapata utambuzi kufahamu dhamira kubwa ya Halifa wa Petro, ambayo daima anatuhimiza kuwa wanafunzi na mitume wa Bwana Mfufuka, ili kwamba watu wote ndani yake wapate Maisha mapya. Kuyachukulia Maisha kama zawadi, na Neema, ni utambuzi wa daima wa kumjua Baba na kuishi katika ushirika naye. Ni hili ndilo msingi wa jamii ya Kikristo ambamo hupata uzoefu na matunda ya imani.
Askofu Mkuu Fisichella aliendelea kueleza kwamba, katika siku hizi mbili, Papa amewawezesha kuiingia katika kiini cha mchakato ulioanzishwa wakati wa Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vatican. Katika hali hii ya mwamko mpya katika Kanisa, kuna hisia kali ya haja ya kushiriki katika Uinjilishaji Mpya, popote Bwana anapo watuma. Kila mmoja wao anajua kwamba upeo wa utume ni kuipeleka Injili kwa wote na kuwafanya kuwa chumvi na mwanga kwa watu wote wake kwa waume.

Askofu Mkuu Fischella alimalizia hotuba yake shukurani kwa Papa kwa maneno ya Mtume Paulo kwa Wakristo wa Efeso: "nawakabidhi kwa Mungu na kwa neno la neema yake, ambayo ni uwezo wa kuwajenga ninyi" (Matendo 20:32) . Safari ni ndefu na yenye changamoto nyingi na ya kuchosha.

Lakini kwa kwa utambuzi wa hayo, tumeweka tumaini letu katika sala za waamini na maongozi ya Papa , kwa ajili ya utume huu wa kuwaleta watu kwa Mungu, na pia kwa misaada ya maombezi ya watakatifu Mwenyeheri Yohane XXIII na Mwenye Heri Yohane Paulo II na pia Mwenyeheri Luigi Novarese, mtangulizi katika njia hii Kanisa Roma, katika harakati ya ya majitoleo ya mateso.

Asante, Baba Mtakatifu. Bwana atawazawadia wafuasi wake uthabiti wa imani kwa wote.








All the contents on this site are copyrighted ©.