2013-05-15 12:09:39

Askofu mkuu Norbert Wendelin Mtega wa Jimbo kuu la Songea ang'atuka kutoka Madarakani!


Baba Mtakatifu Francisko amekubali ombi lililotolewa na Askofu mkuu Norbert Wendelin Mtega wa Jimbo kuu la Songea, Tanzania kung'atuka kutoka madarakani kadiri ya sheria za Kanisa Namba 401 kipengele namba 2.

Wakati huo huo, Baba Mtakatifu amemteua Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa wa Jimbo la Iringa na Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania kuwa Msimamizi wa Kitume wa Jimbo kuu la Songea hadi pale atakapoteuliwa tena Askofu mkuu kushika nafasi hiyo.







All the contents on this site are copyrighted ©.