2013-05-12 14:29:27

Wakristu toeni jibu la wema kwa mabaya- Papa Fransisiko ahimiza.


Jumapili 12 Mei 2013, Papa Fransiko, ameongoza Ibada ya Misa kwa nia ya kuwataja katika daraja la Watakatifu, Wenyeheri wafia dini kadhaa ambao ni Mwenye Heri Antonio Primaldo na wenzake 800 wa Otranto; Mwenye Heri Laura wa Mtakatifu Caterina wa Siena Montoya y Upegui, Sista na mwanzilishi wa Usharika wa Wamisionari wa Maria Asiyekuwa na Doa wa Mtakatifu Catherine wa Siena; Mwenye Heri Maria Guadalupe Garcia Zavala, mwanzilishi mwenza wa Usharika wa Wahudumu wa Mtakatifu Margaret Maria (Alacoque) wa Maskini. .

Tukio hili la kuwataja Wenye Heri hao kuwa ni Wakatifu, lilipitishwa na Baraza la Makadinali (Consistory)hapo tarehe 11 Februari 2013, wakati Papa Benedikto XVI, alipotoa tangazo lake la kihistoria la kujiuzuru kuwa Papa . Watakatifu Mashahidi wa Otranto ni wa Italy na Watawa Masista wawili ni raia wa Amerika ya Kusini.

Akiwatangaza Watakatifu hawa , Mashahidi wa Otranto Italia, Sista Laura Montoya Colombia na Maria Guadalupe GarcĂ­a Zavala, ametoa wito kwa Wakristu wote kuitangaza Injili kwa uaminifu si kwa maneno tu lakini hasa kimatendo, kuushuhudia upendo wa Mungu na upendo Mkristu kwa watu wote kama walivyofanya Mashahidi hawa wa Imani kwa Kristu,ambayo leo wametajwa kuwa mifano bora ya upendo na maisha ya Kikristo. Ni mifano ya uaminifu kwa Kristo .

Katika homilia yake , Papa aliyarejea masomo yaliyo somwa akisema yanatoa wito kwa waamini wote kuwa aminifu kwa Kristo, hata kama ni kuuawa. Na tukio hii la kuwataja Mashahidi hawa wa Imani kuwa Watakatifu, kunaongeza ukurasa mwingine mpya katika kitabu cha Maisha ya Watakatifu yanayo paswa kuingwa na wafuasi wote wa Kristu. Papa alieleza na kurejea hali ya maisha ilivyokuwa katika miaka ya 1480 ambamo watu wa Mashariki ya kati waliishi maisha ya kitisho cha utawala wa Ottoman. Lakini mashahidi wa Otranto kitisho cha kunyongwa, hakikuondoa imani yao kwa Kristu.

Papa alieleza pia kwa kureja imani ya Mtakatifu Stepahno, akisema ni tu katika imani, ambamo tunaweza kuona zaidi ya mipaka ya macho yetu binadamu, zaidi ya mipaka ya maisha ya kidunia, na kuuona ufunuo wa kimbingu na Kristo aliye hai katika mkono wa kulia wa Baba.
Papa aliasa na kutoa wito kwa wabatizwa wote wa kanisa , kutunza imani yao kama kito cha thamani sana, walichopokea. Ni hazina ya kweli, ambayo daima kwa uaminifu wetu kwa Bwana, hufanya upya hata katikati ya vikwazo na kutoelewana. Mungu kamwe hawezi kuacha kutuimarisha na kutupa nguvu na utulivu.








All the contents on this site are copyrighted ©.