Papa amtembelea Kardinali Javier Lozano Barragàn hospitalini
Baba Mtakatifu Francisko, Jumamosi baada ya shughuli zake za kukutana na kuzungumza
na watu mbali mbali, Jumamosi, tarehe 11 Mei 2013, alifunga ofisi na kwenda kumtembelea
Kardinali Javier Lozano Barragàn, Mwenyekiti mstaafu wa Baraza la Kipapa la wahudumu
wa sekta ya afya aliyelazwa kwenye Kliniki ya Pio wa Kumi na moja mjini Roma baada
ya kufanyiwa upasuaji mkubwa.
Baba Mtakatifu ametumia fursa hii pia kusalimiana
na wafanyakazi wa Hospitali hii na kushangazwa na jinsi ambayo Kardinali Barragàn
anavyoyakabili mateso na mahangaiko yake kwa imani na moyo mkuu. Baba Mtakatifu anasema,
kwa hakika Kardinali Barragàn ni kielezo cha ushuhuda wa imani. Itakumbukwa kwamba,
Kardinali javier Lozano Barragàn kutoka Mexico, hapo tarehe 26 Januari 2013 ametimiza
miaka 80 tangu alipozaliwa.