Furaha ya Mkristu ni zaidi ya kufurahia maisha - asema Papa Fransisko
Furaha ya Kikristu ni hija ya furaha ambamo hatuwezi kubaki tumejifungia ndani kwa
ajili yetu wenyewe, vinginevyo tunajiweka katika hatari ya kuwa jamii ya masononeko,
uchungu na majonzi. Aidha furaha ya Mkristu, ni zaidi ya kuwa furaha ya kuchekelea
tu, ila ni furaha iliyosimikwa katika kina cha kiroho. Na si furaha ya kidunia, kwa
sababu msingi wake umesimikwa katika shina la uhakika kwamba Yesu Kristo ni na Mungu
na yuko pamoja nasi. .
Papa Fransisko, alifundisha wakati wa Ibada ya Misa
aliyoiongoza Katika Kanisa dogo la Mtakatifu Marta Vatican ,ibada aliyosaidiana an
Askofu Mkuu Bartazar Enrique Porras Cardozo wa Jimbo la Merida , na pia Askofu Mkuu
Notker Wolf, Mkuu wa Wabenedkitine, ibada iliyo hudhuriwa pia na wafanyakazi wa Redio
Vatican wakiongozwa na Mkurugenzi wa Redio Vatican, Padre Federico Lombardi.
Homilia
ya Papa Fransisko, ililenga zaidi aya kutoka Matendo ya Mitume, ambamo mna maelezo
kwamba, Mkristo iwe mwanamke au mwanamme, anatakiwa kuwa mtu wa furaha . Ndivyo
Yesu anavyotufundisha na pia kanisa hufundisha hivyo. Papa aliendelea kuitafakari
furaha hiyo ya Mkristu akisema, ni zaidi ya furaha ya kawaida kwa kuwa haitokani na
sababu za mpito. Hii ni furaha ya kina ya ndani ya moyo, isiyotokana na mafanikio
ya kidunia, kama sababu za kiuchumi, fedha na kijamii, lakini hii ni furaha inayotokana
na kuuona upeo wa kina wa maisha ya furaha yasiyokwua na mwisho. Ni furaha inayopokelewa
kama zawadi kutoka kwa Mungu, inayojazwa ndani mwetu. Ni upako wa Roho kwamba kwa
hakika Yesu ni pamoja na sisi na pamoja na Baba. "
Aliendelea kusema, mtu wa
furaha, ni mtu wa kujiamini. Ana uhakika kwamba "Yesu ni pamoja na sisi, kwamba Yesu
ni pamoja na Baba. Na alihoji kama ni vyema kuifungia zawasi hii ya furaha ndani
mwetu daima?.
Na alitoa jibu, "Hapana, kwa sababu kama tutaifungia furahi
hii ndani mwetu tu, hatimaye mioyo yetu mioyo yetu itazeeshwa kwa mhemko uliomo ndani
na hivyo kuna hatari za kumezwa na masononeko na huzuni na kuwa na hofu na uzembe,
na kushindwa kuitangaza furaha ya Injili na hili kiroho si afya njema. .Wakristu
ni lazima kuinua kisingino na kuwenda kuitangaza furaha ya Injili kwa kila binadamu.
Nikuifunua mioyo wazi kwa kila mtu ili aweze kuiona furaha hii kamili.. Furaha
hii, ni nguvu ya hija, ni zawadi inayotusindikia katika kuitembea njia ya maisha,
tunapoi tembea na Yesu, kuhubiri, na kuwaleta wote waliolemewa na maisha uchoyo,
ubinafisi, ulafi, ufisadi, ufuska na dhambi nyingine nyingi kwa Yesu. Ni furaha ya
kuwakaribu ndani ya Kanisa wote, ili pia wayaone maisha yao kwa mtazamo wa upeo wa
macho ya Kikristu.
Furaha ni Hija, Papa Fransisko amesisitiza, Mkristo anapo
imba kwa furaha, kinakuw ani kitendo cha kuishuhudia furaha yake inayotoka ndani moyoni
mwake na kuioneysha wazi katika njia ya maisha yake ya kuelekea Mbinguni. Furaha ni
nguvu ya Mkristu katika hija yake , na ni zawadi inayotolewa kwa Ukarimu na Kristu
Mwenyewe pamoja na Roho Mtakatifu.