2013-05-10 10:22:39

Majeshi kutoka Kusini mwa Afrika kuimarisha amani, Mashariki mwa DRC


Afrika ya Kusini, Tanzania na Malawi ni kati ya nchi ambazo zinachangia Askari watakaoshiriki kulinda amani kwenye mpaka kati ya DRC, Rwanda na Uganda, maeneo ambayo kwa miezi ya hivi karibuni yamekuwa ni uwanja wa vita unaodhibitiwa na Kikosi cha Waasi cha M23 kinachoungwa mkono na Serikali ya Rwanda na Uganda, ingawa Serikali zote mbili zimekwisha kanusha tuhuma hizi.

Hivi karibuni Kikosi cha M23 kilitoa vitisho kwa Serikali ya Tanzania na kujibiwa kwamba, Tanzania ni moto wa kuotea mbali, ikithubutu, itakiona cha mtema kuni! Afrika ya Kusini ambayo kwa sasa ina uchumi mzuri inaonekana itachangia zaidi katika masuala ya vifaa vya kijeshi kama njia ya kuimarisha amani huko Mashariki mwa DRC.







All the contents on this site are copyrighted ©.