2013-05-08 12:18:14

Pax Christi yaonesha mshikamano na Waziri Cècil Kyenge


Shirika la Pax Christi nchini Italia linasema limesikitishwa na tabia ya kibaguzi na kejeli zilizooneshwa kwa Waziri Cècil Kyenge wa Italia mwenye asili kutoka DRC na kwamba, kuchaguliwa kwake kuwa ni kati ya Mawaziri wa Serikali inayoongozwa na Waziri mkuu Enrico Letta iwe ni changamoto kwa Italia kutunga sheria itakayowapatia haki watoto wa wahamiaji wanaozaliwa nchini Italia kupewa uraia.

Pax Christi inaungana na watu wote wenye mapenzi mema wanaosimama kidete kupinga ubaguzi wa aina yoyote ile nchini Italia kwa kuzingatia Tamko la Haki Msingi za Binadamu. Changamoto hii inakuja wakati ambapo Kanisa linaadhimisha Jubilee ya miaka 50 tangu Baba Mtakatifu Yohane wa Ishirini na tatu alipochapisha Waraka wa "Pacem in Terris" "Amani Duniani".

Kuna haja kwa Jumuiya ya Kimataifa kujenga na kudumisha sera za ukarimu, amani na utulivu, kwa kukazia haki na wajibu wa kila raia.







All the contents on this site are copyrighted ©.