Uteuzi...Majimbo ya Kokstad na Kabungo yapata Maaskofu
Baba Mtakatifu Fransisko amemteua Padre Zolile Peter Mpambani , kuwa Askofu mpya wa
Jimbo la Kokstad, Afrika Kusini.
Askofu Mteule Zolile Peter Mpambani S.C.I,
alizaliwa 20 Februari 1957 huko Umlamli katika Jimbo la Aliwal. Na alijiunga na Shirika
la Moyo Mtakatifu wa Yesu Januari 28, 1982. Amehitimu ktiak masomo ya Filosofia na
teolojia katika Seminari Kuu ya Mtakatifu Joseph ya Cedaral. Na alipadirishwa tarehe
25 April 1987. Hadi kuteuliwa kwke alikuwa Vika Mkuu wa Parokia katika Jimbo la
Aliwal. Pia Februari aliteuliwa kuwa Mkuu wa Kijimbo wa shirika la Moyo Mtakatifu,
Kanda ya Afrika Kusini. Jimbo la Kokstad lilizinduliwa mwaka 1951 kama sehemu
ya Jimo Kuu la Durban , Lina wakazi 1,809,000 kati yao 85,000ni Wakarìtoliki wanaohudumiwa
chini ya Parokia 16, zinazo ongozwa na Mapadre 21 wakiwa wa jimbo 8 na 13 wa mashirika
ya kitawa,. Kuna Mafrateli 16, Masista 44 na waseminaristi watano . Kiti cha Askofu
cha Jimbo la Kokstad kilibakiwazi Januari 31 baada ya Askofu jimbo hilo kuhamishiwa
katika Jimbo Kuu la Pretoria.
Aidha Papa ameteua Askofu wa Jimbo la
Kibungo Rwanda Baba Mtakatifu amemteua Padre Antoine Kambanda , Gombera
wa Seminari Kuu ya Mtakatifu Charles ya Nyakibanda Butare, kuwa Askofu mpya wa Jimbo
la Kibungo Rwanda.
Askofu Mteule alizaliwa 10 Novemba 1958 jimboni Kigali.
Wazazi wake wote wawili waliuawa wakati wa vita vya mwaka 1994. Alijipatia elimu
ya awali nchini Burundi na Uganda na masomo ya sekondari nchini Kenya. Alisoma masomo
ya filosofia na teolojia nchini Rwanda na kukamilisha elimu ya teolojia katika seminari
Kuu ya Nyakibanda jimboni Butare.
Alipadirishwa Septemba 8 1990 na Mwenye
Heri Papa Yohane Paulo 11, wakati akitembela Rwanda. Na alifanywa kuwa Gombera wa
Seminari Kuu ya Mtakatifu Charles ya Nyakibanda mwaka 2006. Kiti cha Askofu katika
jimbo la Kibungo kilibaki wazi tangu mwaka 2010, baada ya Askofu wa jimbo hilo kustafu
kwa mujibu wa sheria ya Kanisa 401/2..