2013-05-07 15:16:38

Italia yamlilia Giulio Andreotti na hali mchanganyiko


Italia inamlilia Giulio Andreotti., aliyekuwa senata wa maisha, aliyefariki Jumatatu 06 May 2013, asubuhi, nyumbani kwake Roma, akiwa na umri wa miaka 94.

Mwana habari Alessandro Guarasci wa Radio Vatican anabainisha kwamba, kwa miaka 40, Andreotti alikuwa mmoja wa nembo ya siasa Italia. Ingawa hakupendwa na wengi, lakini ameacha mengi ya kukumbukwa, mojawapo ikiwa ni mwanasiasa mkongwe aliyechanguliwa kuingia bungeni akiwa na umri mdogo wa miaka 27 tu . Na aliongoza serikali ya Italia kama Waziri Mkuu kwa mara 7, na kuwa mjumbe wa bunge kwa miaka sitini na sita.

Mazishi ya mwanasiasa huyu mashuhuri Italia , yanafanyika katika hali ya faragha kulingana na matakwa yake. Katika maisha yake ya kisiasa, alikabiliwa na tuhuma mbalimbali,ikiwemo kuhusishwa na kikundi haramu za mafia, tuhuma alizokanusha vikali.

Kardinali Camillo Ruini, akimwelezea Marehemu Giulio Andreotti, amerejesha kumbukumbu zake za zamani, akiwa Katibu wa Baraza la Maaskofu la Italia, alipokutana binafsi na Andreotti mwaka 1986, kwmba , alivutwa na hisia na hekima za Andreotti, ambaye licha ya kuwa mtu mcheshi na mtanashati, pia alijaliwa busara na hekima , asiyeficha maadili ya Kikristo, wala kuificha imani yake Katoliki. Na alikuwa mtu mwerevu aliyejua vyema mbinu za kusawazisha marumbano katika utendaji wa taasisi za kisiasa na imani yake kama Mkristu .


Na rais wa CEI, Kardinali Angelo Bagnasco ametaja umuhimu wa Andreotti kwa Jamhuri ya Italia, kwa kuonyesha matumaini yake kwamba, Italia itaangalia historia ya maisha ya Andreotti na kuyachukua yote yaliyo mema kwa ajili ya manufaa ya taifa la Italia. .








All the contents on this site are copyrighted ©.