Kikosi cha Waasi cha Seleka hivi karibuni kilichoma zaidi ya nyumba 400 na kupelekea
watu 9 kupoteza maisha yao pamoja na kunajisi Kanisa kwenye Kijiji cha Ouango, Jamhuri
ya Watu wa Afrika ya Kati. Inasemekana kikundi hiki kilichosababisha maafa makubwa
kiasi ni kutoka nje ya nchi.
Watu wengi wanaendelea kupoteza matumaini na
kwamba, jitihada za kuanzisha mchakato wa majadiliano ya kidini kati ya Wakristo na
Waislam katika eneo hili bado zinakwama. Mgogoro wa kivita nchini humo unaendelea
kusababisha maafa makubwa kwa watu na mali zao. Watoto wanaendelea kupelekwa mstari
wa mbele katika mapambano haya, jambo ambalo linawanyima watoto hao haki zao msingi.