Afya ya Mzee Madiba yasababisha gumzo Afrika ya Kusini!
Chama cha ANC cha Afrika ya Kusini kimekanusha habari zilizovumishwa na mitandao ya
kijamii iliyokuwa inaushutumu uongozi wa juu wa Chama cha ANC kwa kupiga picha na
Mzee Nelson Mandela mwenye umri wa miaka 94 ambaye kwa sasa anaonekana kwamba, amedhohofu
sana kama kampeni ya kutaka kujijenga kisiasa.
ANC inasema picha zilizopigwa
na hatimaye kusambazwa kwenye mitandao ya kijamii inataka kuwashirikisha watu hali
halisi ya maisha ya Mzee Nelson Mandela kwa sasa na wala si kutaka kumdharirisha kama
wanavyodai baadhi ya watu ndani na nje ya Afrika ya Kusini. Mzee Madiba kwa miezi
ya hivi karibuni hali yake imeendelea kudhohofu kiasi cha kulazimika mara kadhaa kulazwa
Hospitalini kwa ajili ya kupatiwa matibabu zaidi.