2013-04-25 15:18:27

Papa ampigia simu Rais Giorgio Napolitano...


Jumatano majira ya jioni Papa Francisko, alimpigia simu Rais wa Italia Giorgio Napolitano, kwa nia ya kumshukuru kwa telegram ya matashi mema aliyompekea wakati akiadhimisha Siku Kuu ya somo wake, Mtakatifu George, siku ya Jumanne.

Na kwamba amempigia simu, kwa sababu, Rais huyo, amekuwa ni Mfano wa kuigwa katika utendaji wa Rais yeyote, jinsi anavyopaswa, kuiishi misingi ya umoja na ushirikiano na wengine , wakati wa vipindi vya misukosuko na majaribu yanyotaka kuigawa jamii, na jinzi ya kuvishinda vishawishi vya kuzua mizozo na ghasia.
Na Msemaji wa Vatican, anasema kwa mwaka huu, Papa Francisko atafanya ziara moja tu ya Kimataifa Brazil-
Padre Federico Lombardi, Msemaji wa Vatican, amebainisha kwamba, Papa Francisko atakuwa na ziara moja tu ya kimataifa kwa mwaka 2013.
Msemaji huyo ambaye pia ni Mkurugenzi wa ofisi ya habari ya Vatican, Padre Lombardi, aliuambia mkutano wa wanahabari uliofanyika katika makao makuu ya Ofisi ya Chama cha wanahabari cha Roma. Aliwataka wanahabri hao wasitarajie sana matukio ya safari za Kipapa za Kimataifa kwa mwaka huu, zaidi ya safari atakayoifanya Papa Francisko, huko Rio de Janeiro, Julai 23-28, kwa ajii ya Maadhmisho ya SIKU YA vijana ya Dunia , itakayongozwa na Madambiu: “Nendami na Mkawafanye watu wa mataifa yote kuw awanfunzi wangu” (Mt 28, 19).
Na pia msemaji wa Vatican , almeeleza juu ya kuchapishwa kwa waraka wa Kipapa wa kwanza wa Papa Bergoglio, huku akikumbusha kwamba, Mstaafu Benedict XVI, alikuwa tayari ameandaa mengi juu ya mada ya imani, tunayoiadhimisha mwaka huu.
Na kwamba , Papa Mstaafu, ambaye kwa sasa anakaa katika Castel Gandolfo, unatarajiwa kurejea katika makazi yake , katika Monasteri ya Mama wa Kanisa , mwishoni mwa April au Mei mapema. Na Papa Francesco, ataendelea kuishi katika jengo la Mtakatifu Marta, ambako, anajisikia vizuri hadi itakapo tangazwa vinginevyo.
Na pia hivi karibuni mismamizi wa safari za Kipapa Dr. Alberto Gasbarri, ambaye ni msimamizi mkuu katika safari za Papa, yuko katika maandalizi ya safari ya kwenda Rio de Janeiro, kwa ajili ya matayarisho ya ziara ya Papa Francisko. Baba Mtakatifu Francisko atashiriki katika sherehe na Ibada ya Mkesha wa Vijana na njia ya Msalaba kwa ajili ya kufunga adhimisho la Siku ya Vijana ya Dunia kama ilivyopangwa tarehe kufanyika jumapili Julai 28 , katika uwanja wa Imani wa Guaratiba, Brazil.









All the contents on this site are copyrighted ©.