Msijifungie katika ubinafsi, kuweni wazi na sikilizeni wengine!
Katika kipindi hiki cha athari za myumbo wa uchumi kimataifa, watu wengi wanaonekana
kukata tamaa kiasi hata cha kukosa dira katika maisha. Kimekuwa ni kipindi cha taabu
na mahangaiko kwa familia nyingi hasa kutokana na ukosefu wa fursa za ajira, hali
ambayo inakwamisha mipango ya watu wengi, hali ambayo pia imepelekea kumong'onyoka
kwa misingi ya maadili na utu wema. Baadhi ya watu wanatafuta njia za mkato katika
maisha!
Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe wake kwa watumiaji wa mitandao
ya kijamii, twitter anasema kwamba, katika kipindi hiki cha athari za myumbo wa uchumi
kimataifa, hakuna haja mtu kujifungia katika ubinafsi, bali kujiweka wazi na kuwasikiliza
wengine.