2013-04-24 16:29:42

Msingi wa maadili na kipimo cha jamii, ni mahitaji msingi katika maendeleo endelevu


Umuhimu wa kufuta umaskini kama ulivyo azimiwa katika Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) si tu hitaji la kutimiza maazimio ya Mkutano wa Rio+ 20, lakini kimsingi , kuna hitaji la kuzingatia maadili msingi katika kushughulikia namna nyingi za umaskini wa sasa katika familia ya binadamu na chaguo linalo lenga kukuza udugu na amani . Huu ni uchaguzi wenye upendeleo katika kufanikisha juhudi za kutokomeza umaskini kupitia utendaji wa maendeleo endelevu, wenye kuzingatia msingi wa maadili na kipimo cha jamii.
Ni kauli ya Askofu Mkuu Francis A. Chillikutt, Nunsio na mtazamaji wa Kudumu wa Jimbo la Papa katika Umoja wa Mataifa, wakati akihutubia mkutano wa kidharura wa kikundi cha utendaji kwa ajili ya ufanikishaji Maendeleo endelevu ya Millenia, siku ya Jumatatu ya 18 April 2013. Mkutano uliofanyika kwa nia za kubadilishana mawazo juu ya ufutaji wa ufukara duniani.
Askofu Mkuu Chillikutt alisema, kutokomeza umaskini lazima kwanza , kunahitaji uelewa katika mitazamo ya usawa katika utu wa kila mmoja na kila binadamu. Na zaidi sana, juhudi hizo zinapaswa kuongozwa na kanuni za sheria ya asili, yenye kuvuvia maamuzi ya kisiasa , kisheria na kiuchumi na mbinu za utendaji katika sheria za kimataifa.
Ni kuyaweka maendeleo yote ya binadamu, kama kituo kikuu cha juhudi zote za kutokomeza umaskini na uelewa sahihi juu ya umaskini na njia bora za kufuta umaskini huo. Malengo ya maendeleo ya endelevu, kwa hiyo, yanahitaji umuhimu wa utu na heshima ya binadamu kupewa kipaumbele, kwa mujibu wa kutambua maamuzi na kanuni ya kwanza ya maendeleo endelevu, kama ilivyo tolewa na Mkutano wa Rio, 1992, kwa ajili ya uhamasishaji wa mipango ya maana ambayo ni sikivu katika mahitaji ya kila mtu na jamii.
Ili kupitisha malengo ya hatua hiyo yenye mtazamo wa ubinadamu unaozingatia hasa watu maskini na wale walio pembezoni mwa jamii, ambao ni wengi waliokumbwa na wanapaswa kufaidika zaidi - ni lazima sauti yao isikilizwe wakati wa kupanga mipango na utekelezaji.

Askofu Mkuu aliendelea kuzungumzia umaskini unaotokana na watu kutengwa na wengine, katika maisha ya kiuchumi, kijamii, kisiasa na kitamaduni, watu hao wakiwekwa nje ya jamii wanamoishi kama familia moja ya binadamu, wakionekana kama wao hawawezi hawana uwezo wa kuendeleza yaliyo mazuri, na hivyo hunyima fursa muhimu kushiriki wao wenyewe , familia zao na jamii zao, katika maendeleo endelevu.
Askofu Mkuu Chillikutt, katika mitazamo hiyo, amesema, juhudi za kuwabagua maskini katika mipango ya utendaji , inakuwa na maana kuwanyima watu maskini mahalia, sehemu yao halali katika maisha ya familia ya binadamu, na katika matumaini na ndoto za mafanikio yao, ambayo yote mizizi yake imesimikwa katika ubinadamu wetu wa kawaida, na ambayo hakuna hata nchi moja, watu au utamaduni , wanaoweza kudai wana haki kipeee ya umiliki.
Alikumbusha mkutano kwamba, watu wote, kwa sababu ya uanachama wao katika familia ya binadamu, huwa na haki ya uzaliwa na haki ya kunufaika na urithi huu wa kawaida, kuwa ni haki na wajibu wao, kushiriki katika kurutubisha urithi huu mkubwa wa dunia..
Na kwamba mwelekeo wa kutaka kutenga baadhi ya jamii maskini kwa sababu za kutokomeza umaskini, unaweza kuvunjwa kwa njia ya kuwashirikishwa maskini hao , katika utendaji wote wa kiuchumi, kijamii, kisiasa na kiutamaduni, kwa maana ya kuvunja vikwazo vyote, na wote kuingizwa, kila mmoja akiwa na stahili ya kupata marupurupu na faida zote kwa gharama za wote.
Askofu Mkuu Chillikutt alibaini , kutengwa kwa jamii maskini , hukuzwa na ubinafsi katika urithi wa pamoja ya binadamu, kiakili na kiasili hasa kwenye haki za biashara za serikali, na hivyo hujenga usugu wa kiuchumi na siasa tegemezi.
Na kwamba, mipango ya kuwahirkisha wote , kwa upande mwingine, unapata maana kuwakaribisha maskini kushiriki katika mifumo yote ya kiuchumi, kijamii, kisiasa na kiutamaduni kama washirika kamili, na kujenga uwezo wao, ili waweze kuchukua kiti chao katika mezani ya wote, kwa usawa kamili , hivyo kwamba masoko ya kiuchumi, yanakuwa ni kwa ajili ya faida ya wote.
Mtindo huu wa ushirikishaji unapata maana ya kweli ya ubinadamu unaozingatia, mbinu ya kuondoa umaskini na msada unao hakikisha kwamba malengo ya maendeleo endelevu, inakuwa mfano wa kuigwa kwa ajili ya kukuza ushirikiano wenye kuzingatia uzoefu na hekima za wale ambao kila siku wanakabiliwa na hali halisi za changamoto za umaskini na pia ujasiri na uvumilivu wa watu hao.







All the contents on this site are copyrighted ©.