Jifunzeni kutoka kwa Bikira Maria kutambua sauti ya Kristo na kuifuata!
Baba Mtakatifu Francisko anaendelea kupata wafuasi wengi katika akaunti yake ya mtandao
wa kijamii ujulikanao kama twitter. Takwimu zinaonesha kwamba, hadi sasa kuna wafuasi
takribani millioni sita ambao wanamfuata katika akaunti yake. Katika lugha ya Kiingereza
kuna jumla ya wafuasi millioni mbili na laki nne. Taarifa zinaonesha kwamba, wafuasi
wake wanaotumia lugha ya Kihispania kwa sasa wameanza kuongezeka maradufu na kufikia
wafuasi millioni mbili na laki nne na arobaini na sita elfu.
Baba Mtakatifu
Francisko siku ya Jumanne, tarehe 23 Aprili 2013 katika ujumbe wake kwa watumiaji
wa mtandao wa twitter anasema kwamba, Bikira Maria ni mwanamke aliyethubutu kusema
"Ndiyo", awasaidie waamini kutambua sauti ya Kristo na kuifuata.
Baba Mtakatifu
bado anafanya rejea kwenye Maadhimisho ya Jumapili ya Nne ya Kipindi cha Pasaka, maarufu
kama Jumapili ya Kristo Mchungaji mwema, Siku ya kuombea miito mitakatifu ndani ya
Kanisa.