2013-04-23 15:07:02

Papa: Hakuna nafasi ya biashara dini' katika Ufalme wa Mungu



Mapema Jumatatu, Papa Francis aliwaasa,wanaotafuta manufaa binafsi kupitia mgongo wa jamii au dini kwamba , katika dini hakuna nafasi au ngazi ya kupandia kwa nia ya kutaka kujinufaisha mwenyewe kimaslahi au kimamlaka.
Papa alieleza wakati akiongoza Ibada ya Misa katika Kikanisa cha Mtakatifu Marta ndani ya Vatican , ibada iliyohudhuria na Wafanyakazi na waandishi wa habari kutoka Ofisi ya Habari ya Vatican , Redio Vatican na Kituo cha kurushia cha St Maria di Galeria, wakiongozwa na
Homilia ya Papa, ilitazamisha katika Injili, ambamo Yesu anawaambia wanafunzi wake kuwa, yeyote asiyeingia kupitia Mlango wa zizi , si mchungaji, lakini ni mwizi na mnyang'anyi. Hii ina maana yeyote anayetafuta kupata faida zake binafsi,kwa mgongo wa dini na jamii, kupitia njia za uongo na udanyanyifu, hana nafasi katika ufalme wa Mungu. Lango pekee la kuingia Ufalme wa Mungu, na Kanisa, ni kuliishi Neno la Injili ya Yesu mwenyewe.

Papa aliwataja walaghai na mafisadi , ambao wamo hata katika jamii ya Kikristo, wale wenye ubinafsi wa kujiangalia wenyewe tu, kupitia kupitia milango mingine mbalimbali kuwa ni wezi na majambazi. RealAudioMP3







All the contents on this site are copyrighted ©.