2013-04-22 11:03:38

Imani vuguvugu hujenga makanisa madogo lakini si Kanisa la Yesu - Papa Francesco.


Wakristo wenye imani haba au wenye imani vuguvugu, hujenga kanisa katika kipimo chao wenyewe na hivyo hilo si kanisa la Yesu, Papa Francesco, alieleza mapema siku ya Jumamosi, wakati wa Ibada ya Misa, aliyoadhimisha akiwa na watu wa kujitolea kutoka Zahanati za Watoto ya Mtakatifu Marta . Ibada ilifanyika katika Kikanisa cha Domus Sanctae Martha ndani ya Vatican.
Baadhi ya washiriki wakiwa Mabinti wa Upendo wa Paolo wa Mtakatifu Vincent de, Jumuiya ambayo kwa muda wa miaka kwa miaka 90, imekuwa ikisaidia watoto na familia zao bila ubaguzi wa kidini wala utaifa. Papa aliongoza Ibada hiyo akisaidiwa na watoto wawili wa kiume.
Katika homilia yake alitazama zaidi Jumuiya za kwanza za Kikristo, kwamba baada ya mateso, walikiishi kipindi cha amani , wakiimarishana , kutembea pamoja na kukua katika kumcha Bwana, wakiimarishwa na faraja ya Roho Mtakatifu". Papa alieleza kwa kulitazama somo kutoka Matendo ya Mitume akisema, “hiii ni hewa halisi ambamo Kanisa linatakiwa kuishi na kupumua. Ni wote wa kutembea mbele ya Mungu na uwajibikaji.
Papa alihoji iwapo maisha ya Kanisa la Yesu, yana maana ya uwepo tu wa hisia ndogo ndogo za kuabudu, hisia zilizojaa mashakamashaka kwa uwepo wa Mungu. Alitoa jibu Hapana . Kanisa halipaswi kutembea katika hali hiyo ya kushakia uwepo wa Mungu, na wala kuwa na utendaji mbovu wala kuwa maamuzi yasiyomfaa binadamu aliyeumbwa kwa sura na mfano wa Mungu. Wakristu Kama Kanisa mbele ya Mungu, muda wote, ni wakati wa furaha inayobubujika kutoka kwa Roho Mtakatifu, Zawadi kubwa iliyotolewa na Bwana , inayowezesha Kanisa kusonga mbele katika imani thabiti ya Injili .
Hivyo Waristu hao wenye imani vunguvugu, nguvu yao haiwezi kutegemewa kujenga kanisa thabiti la Bwana, kwa kuwa upepo kidogo ukivuma huondoka njiana kupotelea gizani.
Papa Francesco, alipeleka mawazo yake kwa Wakristu wengi , ambao kwa wakati huu wanaendelea kulishuhudia jina la Yesu hata katika hatari za vifo, akisema hawa si Wakristu hewa, lakini wapo na tunaishi nao wakitembea na Yesu katika njia ya Yesu.
Wako tayari kutoa jibu kama la Petro alipoulizwa na Bwana: 'Wewe pia unataka kwenda? Simoni Petro alijibu: `Bwana, Twende kwa nani ? Wewe unayo maneno ya uzima wa milele . Hivyo katika kundi kubwa, bado kuna wale ambao wanajua vizuri kabisa kwamba hawawezi kwenda mahali pengine, kwa sababu tu Yeye, Bwana, ana maneno ya uzima wa milele. "

Papa alihitimisha homilia yake na sala: "Tuombe kwa ajili ya Kanisa, ili liendelee kukua, kuimarika, na kutembea katika imani na faraja ya Roho Mtakatifu. Naomba Bwana utuokoe na majaribu ya 'akili ya kawaida' katika majaribu ya kumnung'unikia Yesu, kwa kuwa ni udhaifu na majaribu ya kashfa.."







All the contents on this site are copyrighted ©.