2013-04-20 10:56:59

Askofu mkuu Samuel Klèda achaguliwa kuwa Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Cameroon


Baraza la Maaskofu Katoliki Cameroon katika mkutano wake wa Mwaka uliofanyika hivi karibuni limemchagua Askofu mkuu Samuel Klèda wa Jimbo kuu la Douala kuwa Rais mpya wa Baraza la Maaskofu Katoliki Cameroon. Askofu mkuu Klèda alipadrishwa tarehe 9 Machi 1986. Akateuliwa kuwa Askofu wa Jimbo Katoliki Batouri wakati wa Maadhimisho ya Jubilee kuu ya Miaka 2000 ya Ukristo.

Amewafundisha, kuwaongoza na kuwatakatifuza Waamini wa Jimbo Katoliki Batouri hadi mwaka 2009 alipoteuliwa na Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, kuwa Askofu mkuu wa jimbo kuu la Douala. Kuanzia mwaka 1997 hadi mwaka 2010 alikuwa ni Makamu wa Rais, Baraza la Maaskofu Katoliki Cameroon. Kwa sasa ataongoza kwa kipindi cha miaka mitatu.







All the contents on this site are copyrighted ©.