Papa anasali kwa ajili ya watu waliofikwa na maafa ya mlipuko Texas, USA
Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe wake kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii maarufu
kama twitter, siku ya Alhamis tarehe 18 Aprili 2013 anawaalika waamini na watu wote
wenye mapenzi mema kusali kwa ajili ya kuwaombea watu walioathirika kutokana na mlipuko
uliotokea kwenye kiwanda cha kutengeza mbolea mjini Texas, Marekani.
Taarifa
za Jeshi la Polisi zinaonesha kwamba, watu 5 hadi 15 wanahofiwa kwamba, wamefariki
dunia kutokana na mlipuko huo na wengine zaidi ya watu 200 wamepata majeraha pamoja
na uharibifu mkubwa wa miundo mbinu. Serikali ya Marekani inaendelea kufanya uchunguzi
ili kubaini chanzo cha mlipuko huo.