Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe wake kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii maarufu
kama twitter anawakumbusha kwamba, kupaa kwa Yesu kwenda mbinguni hakumaanishi kutoweka
kabisa, bali anaendelea kuwepo miongoni mwa wafuasi wake kwa namna mpya na kwamba,
yuko karibu na kila mmoja wao.
Anasema ili kuingia katika utukufu wa Mungu
kunahitaji uaminifu wa kila siku katika kutekeleza mapenzi ya Mungu, hata pale inapobidi
kutolea sadaka kubwa!