Mshikamano wa Papa Francisko na wananchi wa Iran na Pakistan waliokumbwa na tetemeko
la ardhi
Baba Mtakatifu Francisko kwa mara nyingine tena ameonesha moyo wa upendo na mshikamano
wa dhati kwa wananchi wa Iran na Pakistan waliokumbwa na tetemeko la ardhi na hivyo
kusababisha maafa makubwa pamoja na uharibifu wa miundo mbinu. Anamwomba Mwenyezi
Mungu aweze kuwafariji wale waliofikwa na msiba wa kuwapoteza ndugu, jamaa na marafiki
ili waweze kufarijika kwa sala zake.
Anawaombea majeruhi waweze kupona haraka
na kuendelea na shughuli zao za kila siku. Kwa namna ya pekee, Baba Mtakatifu anasema
kwamba, yuko pamoja na wote wanaoteseka kutokana na tetemeko la ardhi lililotokea
siku ya Jumanne tarehe 16 Aprili 2013.