2013-04-09 09:35:58

Kuna watoto zaidi ya 2000 waliopotezana na wazazi wao katika mapigano Jamhuri ya Watu wa Afrika ya Kati


Chama cha Msalaba Mwekundu Kimataifa kinakadiria kwamba, kuna jumla ya wakimbizi 22, 100 kutoka Jamhuri ya Watu wa Afrika ya Kati na asilimi arobaini ya wakimbizi hawa ni watoto wenye umri kati ya miaka miwili hadi kumi na minne, waliopotezana na wazazi wao baada ya machafuko ya kisiasa nchini humo hivi karibuni.

Takwimu za Chama cha Msalaba Mwekundu Kimataifa zinaonesha kwamba, kuna walau watoto ambao ni wakimbizi wapatao laki mbili waliokuwepo kati ya mwezi Januari na Februari mwaka huu. Idadi hii imeongezeka maradufu kutokana na mapambano ya vita kuzidi kupamba moto nchini Afrika ya kati. Hadi sasa wachunguzi wa mambo wanasema, hali bado ni tete!







All the contents on this site are copyrighted ©.