2013-04-06 07:47:57

Mchakato wa kuwatangaza waamini kuwa wenyeheri


Baba Mtakatifu Francisko, hivi karibuni alikutana na kuzungumza na Kardinali Angelo Amato, Mwenyekiti wa Baraza la Kipapa la kuwatangaza waamini kuwa wenyeheri na watakatifu na kumpatia ruhusu ya kuchapisha hati ya mchakato wa kuwatangaza waamini kuwa wenyeheri. RealAudioMP3
Muujiza ambao umethibitishwa ni kutokana na maombi yaliyotolewa kwa Mtumishi wa Mungu Maria Theresa Bonzel, mwanzilishi wa Shirika laWatawa wa Mtakatifu Francisko wa Ibada ya Ekaristi, aliyezaliwa kunako mwaka 1830 na kufariki dunia tarehe 6 Februari 1905.
MASHAHIDI WA IMANI:
Mtumishi wa Mungu Manuel Basulto Jimenez, Askofu wa Jimbo la Jean, Hispania pamoja na wenzake watano waliouwawa kutokana na chuki za kiimani nchini Hispania kati ya mwaka 1936 hadi mwaka 1937.
Mtumishi wa Mungu Jose Maximo Moro Briz na waanzilishi wenzake wanne, Padre kutoka Jimbo la Avilla, Hispania, aliyeuwawa kikatili kutokana na chuki za kiimani Hispania kunako mwaka 1936.
Mtumishi wa Mungu Vladimir Ghika, Padre kutoka Jimbo kuu la Bucharest, Romania, aliyezaliwa kunako mwaka 1873 na kuuwawa kikatiliki kutokana na chuki za kiimani mjini Bucharest tarehe 16 Mei 1954.
Mtumishi wa Mungu Joaquin Jovan Marin na wenzake kumi na wanne kutoka Jimbo la Labourer, Hispania, Mapadre wa Shirika la Moyo Mtakatifu wa Yesu, waliouwawa kikatili kutokana na chuki za kiimani nchini Hispania kati ya Mwaka 1936 hadi mwaka 1938.
Mtumishi wa Mungu Andres kutoka Palazuelo, Mwanashirika wa Ndugu Wadogo Wakapuchini pamoja na wenzake thelathini na mmoja, waliouwawa kikatiliki nchini Hispania kutokana na chuki za kiimani kati ya Mwaka 1936 hadi mwaka 1937.
Mtumishi wa Mungu Giuseppe Girotti, Padre wa Shirika la Wadominikani, aliyezaliwa kunako mwaka 1905 na kuuwawa kikatiliki nchini Ujerumani kunako mwaka 1945 kutokana na chuki za kiimani.
Mtumishi wa Mungu Stefano Sandor, Mtawa wa Shirika la Wasalesiani wa Mtakatifu Bosko, aliyezaliwa huko Hungaria kunako mwaka 1914 na kuuwawa kikatili kutokana na chuki za kiimani, huko Hungaria tarehe 8 Juni 1953.
Mtumishi wa Mungu Rolando Rivi, Mseminari wa Jimbo Katoliki la Reggio Emillia-Guastalla, aliyezaliwa kunako tarehe 7 Januari 1931 na kuuwawa kikatiliki kutokana na chuki za kiimani nchini Italia hapo tarehe 13 Aprili 1945.
Baraza la Kipapa la Kuwatangaza waamini kuwa Wenyeheri na Watakatifu limetambua na kuridhia karama za kishujaa zilizooneshwa na Watumishi wa Mungu wafuatao, ambao nao kwa sasa wanaingizwa katika mchakato wa kutangazwa kuwa ni Wenyeheri. Hawa ni pamoja na:
Mtumishi wa Mungu Eladio Mozaz Santamera, Padre wa Jimbo na Mwanzilishi wa Shirika la Watawa wa Yosefina wa Utatu Mtakatifu, aliyezaliwa kunako Mwaka 1837 nchini Hispania na kufariki dunia huko Plasencia, tarehe 18 Machi 1897.
Mtumishi wa Mungu Manuel Aparici Navarro, Padre wa Jimbo aliyezaliwa kunako mwaka 1902 na kufariki dunia tarehe 28 Agosti 1964.
Mtumishi wa Mungu Moises Lira Serafin, Padre wa Shirika la Roho Mtakatifu na Mwanzilishi wa Shirika la Wamissionari wa Bikira Maria wa Upendo, aliyezaliwa nchini Mexico kunako mwaka 1893 na kufariki dunia tarehe 25 Juni 1950.
Mtumishi wa Mungu Generoso Msulubiwa, Padre wa Shirika la Wamissionari wa Mateso ya Kristo, aliyezaliwa nchini Italia kunako tarehe 6 Novemba 1881 na kufariki dunia mwaka 1969.
Wengine katika Orodha hii ni Mtumishi wa Mungu Olinto Marella, Padre wa Jimbo, kutoka Italia aliyezaliwa kunako mwaka 1882 na kufariki dunia tarehe 6 Septemba 1969.
Mtumishi wa Mungu Antoine Kowalczyk, Bruda wa Shirika la Bikira Maria aliyezaliwa nchini Poland kunako mwaka 1866 na kufariki dunia huko Edmonton, Canada tarehe 10 Julai 1947.
Wa mwisho katika orodha hii ya Waamini walioonesha karama ya kishujaa ni pamoja na Mtumishi wa Mungu Silvia Ferreiro da Silva, wanamke mlei, aliyezaliwa huko Ureno kunako mwaka 1882 na kuitupa mkono dunia kunako tarehe 2 Novemba 1950.








All the contents on this site are copyrighted ©.