Waamini wa Kanisa la Mtakatifu Saturinus kumpokea Kardinali Onaiyekan, hapo tarehe
7 Aprili 2013 mjini Roma
Kardinali John Olorufemi Onaiyekan, Askofu mkuu wa Jimbo kuu la Abuja, Nigeria, aliyeteuliwa
na Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, kunako tarehe 24 Novemba 2012 ataadhimisha
kwa mara ya kwanza Ibada ya Misa Takatifu katika Kanisa alilopangiwa kama Kardinali
Padre, kielelezo cha huduma, umoja na mshikamano na Khalifa wa Mtakatifu Petro.
Idara
ya Liturujia za Kipapa inaonesha kwamba, Kardinali atakabidhiwa Kanisa la Mtakatifu
Saturinus lililoko mjini Roma, Jumapili ya Huruma ya Mungu ambayo kwa Mwaka huu inaadhimishwa
hapo tarehe 7 Aprili 2013.