2013-03-31 11:39:15

Kuporomoka kwa Jengo Dar, wengi wanahofiwa kupoteza maisha!


Juhudi za kuopoa miili ya watu waliofukiwa na kifusi baada ya kuangukiwa na Jengo la Ghorofa kumi na sita, lililoporomoka katika mtaa wa Indira Ghandhi na Barabara ya Morogoro, Ijumaa, tarehe 29 Machi 2013 zinaendelea kwa kusua sua kutokana na ukosefu wa vifaa vya uokoaji.

Hadi kufikia Jumamosi jioni maiti 22 zilikuwa zimeopolewa kutoka kwenye kifusi hiki na inahofiwa kwamba, pengine kuna zaidi ya watu 60 ambao wamefariki dunia baada ya kuangukiwa jengo hili ambalo kwa sasa linafanyiwa uchunguzi na vyombo vya usalama ili kubaini chanzo chake nini!

Wahandisi na Makandarasi wanapaswa kufanya kazi zao kwa kuzingatia sheria, maadili na weledi ili kupunguza kama si kusitisha kabisa ajali kazini. Fedha ikitangulizwa mbele na kubeza maisha na utu wa mwanadamu, kuna hatari kubwa ya majengo kama haya kuendelea kuporomoka, kama hofu inayoendelea kutanda kwa jengo pacha karibu kabisa na mahali ambapo ajali hii imetokea.







All the contents on this site are copyrighted ©.