Idadi ya waliofariki dunia Dar inazidi kuongezeka!
Idadi ya watu waliofariki dunia kutokana na kuporomoka kwa Jengo lenye ghorofa 16,
hadi kufikia Jumamosi asubuhi ni watu 17, kadiri ya taarifa ya Mkuu wa Mkoa wa Dar
es Salaam Bwana Said Meck Sadick kwa Shirika la Habari la Reuters. Juhudi za kuokoa
maisha ya watu waliofukiwa na kifusi zinaendelea, ingawa matumaini ya kuwapata wangali
hai yanazidi kufifia kadiri muda unavyozidi kuyoyoma.
Kufuatia tukio hili la
kusikitisha, Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania ametembelea eneo la tukio na kuhuzunishwa
na maafa yaliyotokea. Ametoa agizo ya kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria wahusika
wakuu yaani: mjenzi, mhandisi mshauri na mhandisi wa Jiji aliyetoa kibali pamoja
na mmiliki wa jengo hilo.