Papa Francisko anatwitter na watumiaji wa mitandao ya kijamii!
Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe wake kwenye mtandao wa twitter anawakumbusha
waamini kwamba, ili kuendelea kuwa na Yesu, kuna haja ya kujitoa katika ubinafsi na
hali ya kuiishi imani kwa hali ya kuchoka na mazoea.
Ili kuishi vyema Maadhimisho
ya Juma kuu, kuna haja ya kuingia katika mantiki ya Mungu, inayofumbata upendo na
majitoleo binafsi.