2013-03-26 07:40:03

Salam na matashi mema kutoka kwa Papa Francisko kwenda kwa Wayahudi wa Roma wanapoadhimisha Siku kuu ya Pasaka


Baba Mtakatifu Francisko katika Maadhimisho ya Siku kuu ya Pasaka ya Wayahudi, amemwandikia ujumbe wa matashi mema Rabbi Riccardo Segni, Mkuu wa Jumuiya ya Wayahudi mjini Roma, akisema kwamba, siku chache zilizopita, walibahatika kukutana mjini Vatican, anamshukuru kwa uwepo wake wakati alipokuwa anaanza utume wake kama Khalifa wa Mtakatifu Petro na Askofu wa Roma.

Baba Mtakatifu Francisko anachukua fursa hii kutuma salam na matashi mema kwa Jumuiya ya Wayahudi walioko mjini Roma wakati huu wanapoadhimisha Pasaka ya Wayahudi, inayojulikana kama Pesach! Mwenyezi Mungu aliyewakomboa watu wake kutoka utumwani Misri na kuwaongoza katika Nchi ya ahadi, aendelee kuwakomboa kutoka katika kila aina ya ubaya na kuwaongoza kwa njia ya baraka zake.

Baba Mtakatifu Francisko anawaomba Wayahudi wa Roma kumwombea na kwamba, anawahakikishia sala zake. Ni matumaini ya Baba Mtakatifu Francisko kwamba, wataendelea kujenga na kuimarisha uhusiano huu katika heshima na urafiki.







All the contents on this site are copyrighted ©.