2013-03-25 07:21:50

Wanawake ni vyombo vya upatanisho, haki na amani katika Jamii


Mama Tunu Mizengo Pinda, Mke wa Waziri mkuu wa Tanzania, hivi karibuni alibahatika kutembelea Radio Vatican na kujionea shughuli zinazoendeshwa na Radio hii katika medani mbali mbali za maisha ya mwanadamu. RealAudioMP3

Hili ni jukwaa la majadiliano ya kidini na kiekumene kati ya waamini wa dini na madhehebu mbali mbali. Ni sauti ya wanyonge, inayopania kukuza na kudumisha haki msingi za binadamu, upendo, amani na mshikamano wa dhati, ili dunia iwe ni mahali pazuri zaidi pa kuishi.

Katika mahojiano na Radio Vatican, Mama Tunu Pinda anawaalika wanawake kwa namna ya pekee, kujenga na kudumisha misingi ya haki, amani, upendo na mshikamano, kwa kuanzia katika familia zao. Hii inatoka na ukweli kwamba, Mama ni mdau wa kwanza katika kulinda na kudumisha misingi bora ya maisha tunu za kifamilia.

Anasema, Familia zinaweza kutekeleza dhamana na wajibu wake, ikiwa kama zitakuwa zimesimikwa katika uchaji wa Mungu, maadili na utu wema. Malezi makini ya watoto hayana budi kuanzia katika Familia, kwani Familia imara na thabiti ni nguzo ya Jamii imara na chemchemi ya viongozi bora na shupavu wanaoweza kujitoa kikamilifu kwa ajili ya ustawi na maendeleo ya wananchi wao.

Mama Tunu Mizengo Pinda anawaalika wanawake kwa namna ya pekee, kusimama kidete kulinda na kutetea haki, amani, upendo na mshikamano wa dhati ndani ya Familia, wao wenyewe wakiwa mstari mbele.








All the contents on this site are copyrighted ©.