2013-03-22 15:49:27

Papa Francis akutana na Mabalozi Vatican


Ijumaa hii majira ya saa za asubuhi, katika chumba cha Mikutano,katika jengo la Kipapa , Baba Mtakatifu Francis, alikutana na Mabalozi wanaowakilisha nchi mbalimbali kwa Jimbo Takatifu, ikiwa ni mara yake ya kwanza kukutana na mabalozi hao tangu azindue utume wake katika kiti cha Petro, Jumanne ya wiki hii.
Kwa niaba ya Mabalozi wote, Salaam za Mabalozi kwa Papa, ziliwasilishwa na Balozi Mheshimiwa Jean-Claude Michel, ambaye ni mwakilishi wa Ufalme wa Monaco, katika Jimbo Takatifu, ambaye kwa wakati huu ni Mkuu wa zamu katika chombo kinacho waunganisha Mabalozi. Kwa wakati huu Jimbo la Papa lina mahusiano ya Kidplomasia na mataifa 180.
Papa aliianza hotuba yake kwa Mabalozi , na salaam za shukurani za dhati kwa Waheshimiwa wote , Mabibi na Mabwana,akiutaja wakati huo, kuwa ni nafasi au mwanya mzuri wa kubadilishana salaam za matashi mema na mawazo katika namna ya kawaida, huku ndani mwake, akiwa bado na hisia hai za wakati wa sherehe ya kuzindua kazi na utume wake wa Kipapa, ambamo kwa namna fulani, iliyo toa picha kwamba, Utume wa Kipapa ni kwa ajili ya dunia nzima. Na sasa uwepo wa Mabalozi hao, pia alijisikia kuwa karibu na watu wote wanao wawakilisha, katika kushirikishana furaha na matatizo , matazamio na hamu zao.
Na kwamba , uwepo wa Idadi hii kubwa ya Mabalozi ni ishara kwamba, mahusiano kati ya nchi zao na Jimbo la Takatifu, yana matunda mazuri na yenye faida kwa wanadamu.
Alitaja kwa hakika hilo ndilo lengo na tazamio kubwa kwa Jimbo Takatifu, uwepo wa mazuri kwa ajili ya kila binadmau duniani. Na ni kwa uelewa huo, kwamba Askofu wa Roma , anaanza utume wake, kwa kuweka matumaini yake katika uwepo wa urafiki na maelewano na nchi wanazo wakilisha, na uhakika kwamba wanashirikishana katika lengo hili la kujenga urafiki. Na wakati huohuo , pia ameonyesha kuwa na matumaini ya kupatikana nafasi, wakati huu anapoianza safari hii ya utume wake , ya kwua na mawasiliano na mataifa machache ambayo bado hayajaweka mkataba wa mahusiano ya Kidiplomasia na Jimbo Takatifu, ambayo baadhi yake yalikuwepo wakati wa Ibada ya Misa kwa ajili ya kuzindua utume wake. Na pia wale waliotuma ujumbe wao kama ishara ya ukaribu wao. Kwao wote amewashukuru kwa dhati kwa hilo.
.
Na kwa mara ingine , Papa Francis alirudia, kuwaeleza Mabalozi kwa nini amechagua jina la Francis, mtu maarufu nchini Italia na Ulaya , hata kwa watu wasiokuwa wafuasi wa Kanisa Katoliki , kwamba Francis aliyaacha maisha ya kifahali na kuchagua maisha ya mtu maskini wa mitaani.
Papa amehoji, ni watu wangapi leo hii ambao bado wanaisha katika hali ya umaskini dunia! Na kwa jinsi gani wanavumilia mateso haya makali. Alileleza hilo na kutaja mfano wa Francis wa Assisi, akisema, Kanisa ssehemu mbalimbali za dunia, hujitahidi kuyafuta maisha haya ya Francis kupitia utendajiw a vyombo vyake mbalimbali, vinavyo shughulika na kujali hali za watu mbambali wanao kabiliwa na mateso haya, ambao ni wazi wako katika nchi nyingi, kama wanavyoweza kushuhudia, matendo ya ukarimu unaofanywa na Wakristo, wanao jitolea kusaidia wagonjwa, yatima, wasio na makazi na wanyonge waliosahaliwa na kutengwa pembezoni , wakihangaika kuijenga jamii katika ubinadamu zaidi na haki zaidi.

Pamoja na hilo Papa Francis ameasa kwamba, pia kuna aina nyingine ya umaskini! Ni umaskini wa kiroho wa wakati wetu, ambayo unaathiri hasa nchi zinazoitwa mataifa tajiri. Ni kile mtagulizi wake Mpendwa Benedict XVI, ilicho kiita "ukorofi wa ukana Mungu , wenye kuona mambo yote ni ya mpito “, binadamu akijiamini kuwa na uwezo kwa yote na hivyo kuhatarisha mshikamano wa watu. Na hiyo ni sababu ya pili ya kuchagua jina la Francis. Francis wa Assisi, hata leo hii, anatuambia sisi kwamba , lkazi ya kujenga amani ni ya lazima. Lakini, hakuna amani ya kweli bila ukweli! Na haiwezekani kuwa na amani ya kweli, ikiwa kila mtu anajiona amejikamilisha mwenyewe, na kupuuza utendaji wa mema kwa ajili ya wengine . Kila mtu anapaswa kukumbuka kwamba ni asili msingi ya kila mtu, kuungana na kuwa na mshikamano na binadamu wengine.
Papa aliendelea kueleza , Moja ya cheo cha Askofu wa Roma, Baba Mtakatifu, Mjenzi wa madaraja kati ya Mungu na watu. Na hivyo alionyesha matumaini yake kwamba, mazungumzo kati yao, lazima yataweza kuwa msaada katika ujenzi wa madaraja ya kuunganisha watu wote, kwa namna ambayo kila mtu anaweza kumwona mwingine si adui, au si mpinzani, lakini ndugu, kaka au dada, anayepaswa kupokelewa na kukubatiwa. Kwa maana hiyo, asili ya kazi yake inamsukuma kuwa mjenzi wa madaraja, kutoka pande zote za dunia, ambazo kwa wakati huu, zimezidi kukaribiana na kutegemeana zaidi katika hitaji la kukutana na kutengeneza nafazi za wazi zaidi kwa ajili ya mshikamano na udugu wa kweli.
Kwa ajili ya kazi hii, utendaji wa kidini, unakuwa msingi. Haiwezekani kujenga madaraja kati ya watu na kumsahau Mungu. Na kinyume chake pia ni ukweli, haiwezekani kuwa na mahusiano ya karibu na Mungu na kuwapuuza watu wengine. Kwa hiyo ni muhimu kuimarisha mazungumzo kati ya dini mbalimbali, na Papa anafikiria hasa mazungumzo na Uislamu.
Papa ameendelea kueleza kwamba, alifurahia sana uwepo wa viongozi wengi wa kiraia na kidini kutoka ulimwengu wa Kiislamu, wakati wa Ibada ya Misa ya kuzindua Utume wake. Na pia ni muhimu kuimarisha haja ya kuwafikia wasio waumini, hivyo kwamba tofauti zinazotenganisha na kuuumiza ubiadamu zisiendelee kuwepo. Badala yake itawala hamu ya kujenga madaraja ya urafiki wa kweli kati ya watu wote licha ya utafuti wao.
Kupambana na umaskini, katika yote mawili kihali na kiroho , ujenzi wa amani na madaraja haya, kama ilivyokuwa, awali, vinakuwa ni vituo rejea, katika safari yake ya Kitume aliyoianza, kwa kutoa wito na mwaliko kwa kila nchi iliyo wakilishwa ,kujiunga. Na ameonyakwamba, safari hii, inaweza kuwa safari ngumu, iwapo hawata jifunza kukua katika upendo kwa ajili ya dunia hii. Hili linasaidia pia kufikiria jina la Francis, ambaye anatufundisha kuwa na heshima kubwa kwa uumbaji mzima na katika kuwa walinzi wa mazingira yetu, ambayo mara nyingi, badala ya kutumika kwa ajili ya mema ya wote, wachache wanakuwa tabia za uyonyaji na uchoyo binafsi, usiojali madhara na hasara zinazo tokea kwa wengine.

Papa Francis , alimalizia hotuba yake , kwa kuwashukuru Mabalozi wote wanaofanyakazi sambamba na Sekretariati ya Nchi ya Vatican, kwa kazi ya kujenga amani na madaraja ya urafiki na udugu. Kupitia kwao, alitoa tena shukurani zake za dhati kwa ushiriki wao katika maadhimisho ya juu ya tukio la kuchaguliwa kwake, na alionyesha tena hamu yake ya dhati katika jitihada za kazi kwa ajili ya kutoa matunda ya mema. Na mwisho aliwapa baraka zake za Kipapa akiwaombea neema tele za Mungu ziwafikie wao na familia zao na watu wao wanao wawakilisha Asante!








All the contents on this site are copyrighted ©.