2013-03-21 15:29:43

Wakristu Uarabuni , wafuahia kuundwa kwa Baraza la Kiekumene ...


Kuzaliwa kwa Baraza la Makanisa ya Kikristu nchini Misiri, inatajwa kuwa hatua muhimu ya kiekumeni na msingi kwa Wakristu wa Misri. Baraza hili liliundwa mwishoni mwa Wiki ya Sala ya Kuombea Umoja wa Wakristu wiki lililokamilika a tarehe 10 Februari, kutokana na kuahirishwa katika tarehe zake , kwa sababu za machafuko ya kisiasa Misri.

Askofu Mouneer Hanna Anis, Askofu wa Dayosisi ya Kianglikana Misri, Afrika Kaskazini na Pembe ya Afrika, ameeleza, kuundwa kwa Baraza la Makanisa la Kikristo hivi karibuni ni tumaini kubwa katika uwepo wa umoja wa Wakristu katika nchi za kiarabu. ..Baraza hilo ni chombo cha ushauri, na kimefanikishwa kuanzishwa kwa juhudi za Patriaki Tawadros II wa Kanisa la Kiotodosi.

Kulingana na Askofu Anis, pia Mkuu wa Dayosisi ya Kianglikani ya Yerusalemu na Mashariki ya Kati, pia ametoa mchango mkubwa na muhimu katika kufanikisha juhudi hizi za kuonyesha uwepo wa makanisa na jumuiya za Kikristu katika mataifa haya ya kiarabu, na hivyo wanapaswa kuunganisha nguvu kama jumuiya moja ya Kanisa, kukabiliana na changamoto nyingi zinazo wakabili wakati huu wa hali ya sasa ya mivutano kuongezeka, baada ya utawala wa Husein Mubarak.

Mkutano wa kwanza wa Baraza ulifanyika mwezi uliopita na katika Kanisa Kuu la Kanisa St Mark Coptic Orthodox, ambalo huchukuliwa kama Kanisa Mama katika Makanisa ya Misri.. Katika mkutano huo, wawakilishi wa kutoka Makanisa matano na jumuiya zote za Kanisa, zilihudhuria, waotodosi, Waanglikani, Wakoputiki, Wakatoliki, kutoka makanisa ya kiinjili na makanisa ya Kigiriki pia.

Lengo lake la kwanza la Mkutano kama alivyoeleza Askofu Katoliki la Kikoputiki , Assiut Kiryllos William, ilikuwa ni kuimarisha uhusiano wa upendo na roho ya ushirikiano kati ya makanisa wanachama. Ni kuwa na Mwili mpya wa Kanisa Uarabuni. Askofu wa Assiut Kiryllos William, wakati akihojiwa na shirika la habari la Fides alieleza hayo na kuongeza kwamba chombo hicho kitawasaidia kutembea pamoja katika njia ya uekumene na katika kuwa na msimamo wa pamoja katika mazungumzo na mshikamano na jumuiya zingine zisizo za kikristo. Hii ni fursa nyingine ya kukuza mipango ya pamoja hata kijamii na kitamaduni.

Hata hivyo, aliongeza, lengo sio kutafuta mamlaka ya kisiasa, lakini ni mshikamano wa ndani wa maisha ya makanisa na mtu binafsi.








All the contents on this site are copyrighted ©.