2013-03-21 10:58:29

Siku ya kwanza ya furaha kimataifa 2013


Umoja wa Mataifa kwa mara ya kwanza siku ya tarehe 20 Machi 2013 imeadhimisha Siku ya Furaha Kimataifa, baada ya kupigiwa kura na hatimaye, kupitishwa na nchi wanachama 193 wa Umoja wa Mataifa. Licha ya taabu, mahangaiko na hali ya kukata tamaa inayowakabili watu kutoka sehemu mbali mbali za dunia, lakini pia Jumuiya ya Kimataifa walau inaweza kuonesha furaha hata kwa dakika chache.

Hii inaweza kuwa ni furaha inayofumbatwa kitaifa, katika Jamii, mahali pa kazi, lakini zaidi katika Familia, ambayo kweli inapaswa kuwa ni chimbuko na chemchemi ya furaha; lakini wakati mwingine mambo yanakwenda kinyume na matarajio ya wengi.

Kila mtu anachangamotishwa kuwa ni sababu ya furaha na faraja kwa jirani yake, kama alivyosema Baba Mtakatifu Francisko kwa waamini na watu wote wenye mapenzi mema.







All the contents on this site are copyrighted ©.