2013-03-20 09:42:47

Upembuzi yakinifu kuhusu matumizi ya wanajeshi wa kukodiwa na makampuni binafsi ya ulinzi katika migogoro ya kivita!


Umoja wa Mataifa unafanya upembuzi yakinifu kuhusu matumizi ya wanajeshi wa kukodiwa na makapuni binafsi ya ulinzi na matokeo ya utafiti huu yanatarajiwa kuwasilishwa kwenye Mkutano mkuu wa Umoja wa Mataifa utakaofanyika mwaka 2014.

Haya yamesemwa na Bwana Anton Katz, mtaalam wa masuala ya haki msingi za binadamu anayefanya kazi kwa kushirikiana na Umoja wa Mataifa, baada ya mkutano wao uliofanyika hivi karibuni mjini Geneva.

Kumekuwepo na ongezeko kubwa la wanajeshi wa kukodiwa na makampuni binafsi ya ulinzi ambayo kwa sasa yanafanya kazi katika soko la kimataifa, hali ambayo imechangia kwa kiasi kikubwa kinzani na migogoro ya kivita inayoendelea katika nchi kama vile Syria. Nchi kama Ghana, Mauritius na Togo kutoka Afrika zinataka kufahamu watu wanaojihusisha na biashara hii, ili waweze kuchukuliwa hatua za kisheria.







All the contents on this site are copyrighted ©.