2013-03-18 11:25:36

Wananchi wa Zimbabwe wapiga kura ya maoni kwa amani na utulivu


Wananchi wa Zimbabwe, wapatao millioni mbili, Jumamosi tarehe 16 Machi 2013 walipiga kura ya maoni kuhusu Katiba Mpya ya Zimbabwe inayopania kupunguza madaraka ya Rais na kuimarisha utawala wa sheria na haki msingi za binadamu.

Akizungumzia kuhusu mwitiko wa wananchi katika mchakato wa kupiga kura ya maoni, Jaji Rita Makarau kutoka Tume ya Uchaguzi alisema kwamba, wananchi wachache wamejitokeza kupiga kura katika vituo 9,400 vilivyokuwa vimepangwa. Zimbabawe ina wananchi millioni 6.6 waliokuwa wamejiandikisha kupiga kura ya maoni, ingawa vyama vikuu vya kisiasa vilikuwa vimekubali kushiriki katika mchakato wa kupiga kura.

Zoezi la kuhesabu kura za maoni limeanza na linatarajiwa kukamilika walau baada ya siku tano. Wananchi wengi wameshiriki kwa amani na utulivu.







All the contents on this site are copyrighted ©.