2013-03-18 11:37:14

Unyanyasaji wa kijinsia ni kosa la jinai linalopaswa kushughulikiwa kisheria


Kardinali Wilfrid Fox Napier wa Jimbo kuu la Durban, Afrika ya Kusini, ameomba msamaha kwa wote walioguswa na kutendewa na kauli yake kwamba, watu wanaofanya vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia na ni wagonjwa na wanahitaji kupewa tiba, bila ya kukazia kwamba, ni vitendo vya jinai ambavyo vinapaswa kushughulikiwa kisheria.

Kardinali Napier anasema, pengine Kanisa Katoliki halikutoa uzito mkubwa kwa vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia pamoja na kuchukua hatua za kuvikomesha, kwani madhara yake yamekuwa ni makubwa mno katika maisha na utume wa Kanisa, sehemu mbali mbali za dunia. Watu walionyanyaswa kijinsia wanahaki ya kupata msaada wa hali na mali kutoka kwa Kanisa, wanapojitahidi kuponya madonda na maumivu yao ya ndani.







All the contents on this site are copyrighted ©.