Rais Yoweri Museveni wa Uganda ameungana na wakuu mbali mbali wa nchi na Jumuiya ya
Kimataifa wanaoendelea kutuma salam za matashi mema kwa Baba Mtakatifu Francis kwa
kuchaguliwa kwake kuliongoza Kanisa Katoliki lenye waamini zaidi ya Billioni 1.2,
walioenea sehemu mbali mbali za dunia.
Rais Museven anatambua na kuthamini
mchango uliotolewa na Baba Mtakatifu Francis ambaye kwa sasa wengi wanamwita Baba
Mtakatifu wa Maskini, katika maisha yake. Anamwomba, atumie uzoefu na mang’amuzi yake
kutoka katika nchi za kimissionari ili kuleta mabadiliko ndani ya Kanisa.
Lakini,
hata hivyo Rais Museveni habainisha wazi wazi mabadiliko ambayo angependa Baba Mtakatifu
Francis ayafanye kwa ajili ya ustawi, mafao na maendeleo ya Kanisa na Jamii kwa ujumla.