2013-03-16 11:24:38

CELAM wanamhakikishia Baba Mtakatifu Francis mshikamano wa kidugu katika utekelezaji wa majukumu yake kama Khalifa wa Mtakatifu Petro


Shirikisho la Mabaraza ya Maaskofu Katoliki Amerika ya Kusini na Caraibi, katika maadhimisho ya Mwaka wa Imani, limemtumia salam na matashi mema Baba Mtakatifu Francis kwa kuchaguliwa kwake kuliongoza Kanisa Katoliki.

Wanamshukuru Mwenyezi Mungu kwa kulijalia Kanisa kiongozi mkuu wa Kanisa ambaye amevuta hisia za wengi tangu wakati wa uchaguzi wake hadi alipotangazwa hadharani. Yote haya yamefanyika katika kukuza na kudumisha mshikamano katika shughuli za kichungaji na Khalifa wa Mtakatifu Petro. Maaskofu wa CELAM wanasema kwamba, kwa hakika, anaonesha zile changamoto za ugunduzi, ari na moyo wa kimissionari.

Huu ni mwanzo wa hija ndefu kati ya Askofu na Familia ya Watu wa Mungu Jimboni Roma, Kanisa linalohifadhi kwa namna ya pekee, umoja na upendo. Ni hija ya udugu, upendo na imani kati yao wote. Ndiyo matashi ya Maaskofu Katoliki kutoka CELAM.







All the contents on this site are copyrighted ©.