Salam za pongezi na Matashi mema kutoka katika Umoja wa Mataifa
Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bwana Ban Ki-Moon amemtumia salam za matashi mema
Baba Mtakatifu Francis kwa kuchaguliwa kwake kuliongoza Kanisa Katoliki. Ni matumaini
yake kwamba, Umoja wa Mataifa utaendelea kushirikiana na Papa Francis, katika utekelezaji
wa mchakato wa kutafuta na kudumisha misingi ya amani, haki jamii pamoja na haki msingi
za binadamu, kama nguzo msingi za maendeleo endelevu.
Umoja wa Mataifa una
amini kwamba, changamoto mbali mbali zinazojionesha duniani zinaweza kukabiliwa kwa
njia ya majadiliano. Ni matumaini ya Bwana Ban Ki-Moon kwamba Baba Mtakatifu Francis
ataendeleza urithi na utajiri mkubwa ulioachwa na Papa mstaafu Benedikto wa kumi na
sita katika mchakato wa kuendeleza utamaduni wa mshikamano.