Kardinali Jean Louis Pierre Tauran, Rais wa Baraza la Kipapa la Majadiliano ya Kidini
ndiye aliyepewa dhamana ya kumtambulisha na kumtangaza Papa Mpya kwa waamini waliokuwa
wamemiminika kwenye Uwanja wa Kanisa kuu la Mtakatifu Petro, mjini Vatican. Kardinali Tauran
anatoka katika kundi la Makardinali Mashemasi. Yeye ndiye mwenye umri mkubwa. Anapewa
pia dhamana ya kumvisha Palio Takatifu, Baba Mtakatifu Mpya. Kardinali Tauran alianza
kutumikia dhamana tangu tarehe 21 Februari 2011. Tunawatangazia furaha kubwa, kwamba,
tumempata Papa Mpya! Giorgio Bergoglio, SJ. amechagua kuitwa Francis wa kwanza
kutoka katika Shirika la Wayesuit. Ana umri wa miaka 77.