2013-03-13 09:12:49

Kikundi cha Waasi cha Seleka, Jamhuri ya Afrika ya Kati kinatishia maisha!


Askofu Juan Josè Aguirre Munos wa Jimbo la Bangassou, Jamhuri ya Afrika ya Kati anasema kwamba, machafuko ya kivita yanayoendelea nchini mwake yanaendelea kusababisha madhara makubwa kwa watu na mali zao.

Kikundi cha Waasi wameanza kufanya uvamizi na kupora mali za watu na Kanisa na kuelekea mpakani na Sudan. Lengo la kikundi hiki cha waasi ni kutaka kuipindua serikali na kuanzisha serikali itakayosimamiwa na sharia za dini ya Kiislam.

Kujiimarisha kwa kikundi hiki kunaonekana kwamba, kinapata msaada wa hali na mali kutoka nje ya nchi kwa malengo binafsi, kama inavyojionesha nchini Mali. Ingawa kuna vikosi vya kulinda amani kutoka Mali na Afrika ya Kusini, lakini Kikundi cha Waasi wa Seleka linadhibiti asilimia 80 hadi 90% ya nchi ya Afrika ya Kati. Kikundi hiki kinaendelea kuleta uharibifu mkubwa katika miundo mbinu na nyaraka, kiasi kwamba, historia ya wananchi wengi iko mashakani.







All the contents on this site are copyrighted ©.