Sala ya waamini kwa ajili ya kuombea uchaguzi wa Papa Mpya
Waamini kutoka sehemu mbali mbali za dunia waliungana na Makardinali kwa ajili ya
kusali ili kuombea uchaguzi wa Papa Mpya. Katika Sala za Waamini, wamesali kwa ajili
ya kuliombea Kanisa mchumba wa Kristo, ili liweze kudumu katika ukweli, utakatifu,
umoja na amani.
Mwenyezi Mungu
awajalie Makardinali mapaji ya Roho Mtakatifu; awajalie akili na ushauri, hekima na
mang'amuzi. Watu wote washirikiane kwa ajili ya mafao ya wengi, kwa kudumisha haki,
amani, utulivu na mshikamano. Awafariji wote wanaoteseka na kudhulumiwa bila kuwasahau
waliokata tamaa! Awaimarishe waamini katika utii na unyenyekevu, wajitoa sadaka na
kuonesha upendo wa dhati.
Sala ya Waamini kwa Lugha ya Kiswahili kwa ajili
ya kuombea mchakato wa uchaguzi wa Papa Mpya imetolewa na Sr. Martha Msambiri, kutoka
Shirika la Masista wa Upendo wa Bikira Maria Mkingiwa Dhambi ya Asili la Ivrea.