2013-03-05 16:11:34

Kikao cha Tatu cha Makadinali : hakuna tarehe iliyopangwa ya conclave.


Padre Federico Lombardi, Jumanne majira ya saa saba alitoa muhtasari kwa wanahabari katika kile kilicho endelea katika Mkutano wa kawaida wa Makardinali kwa ajili ya maandalizi ya Kikao cha "conclave" cha kumchagua Papa Mpya .
Mkutano huo kwa wanahabari ulifanyika katika Ofisi ya Habari ya Vatican. Padre Lombardi, alitaja mambo muhimu yaliyofanyika kwamba, asubuhi Jumanne, Makardinali, walituma ujumbe kwa Benedict XVI. Na kwamba bado maamuzi hayajafanyika juuya tarehe ya kuanza vikao vya Conclave.
Jumatatu jioni, Makardinali walisikiliza, tafakari ya Neno la Mungu kutoka kwa Mhubiri katika jengo la Kipapa, Padre Raniero Cantalamessa.
Padre Federico Lombardi pia amesema, Makardinali waliofika Roma , Jumatatu jioni, ambao hawakuwepo katika kikao cha Asubuhi, walifanya kiapo chao wakati wa kikao cha jioni, hasa wapiga kura, Kardinali Rai, wa Upatrikai wa Lebanon ya Maronite Kardinali Meisner, Askofu mkuu wa Cologne, Kardinali Völki, Askofu Mkuu wa Berlin, Kardinali Sarr, Askofu Mkuu wa Dakar na pia Kardinali Duka , Askofu Mkuu wa Prague. Na jana iliamuliwa kwamba, watakuwa na vikao wakati wa asubuhi tu kwa Jumanne na Jumatano.
Jumanne asubuhi, wakati wa Kikao cha tatu kimefanyika kati ya 9.30 na 12.40, ambamo baadhi ya Makardinali waliowasili Jumanne, wenye haki ya kupiga kura, walikula kiapo chao. Nao ni Kardinali Rouco Varela na Kardinali Grocholewski. Na hivyo, hadi nyakati za mchana, Makadinali wapiga kura walikuwa 110 katika kusanyiko hilo la Makardinali 148 waliofika kwa mkutano huo .
Na kwamba, katika kikao cha tatu asubuhi, michango 11 ilitolewa na Makadinali kwa mada za mkutano , ikwemo shughuli za Jimbo Takatifu na idara zake mbalimbali, uhusiano wa Makardinali na Maaskofu, upya wa Kanisa katika mwanga wa Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vatican, hali ya Kanisa na mahitaji ya uinjilishaji mpya katika ulimwengu, na hali tofauti za kitamaduni. Na kwamba , katika yote, kati ya jana na leo, kuliwakilishwa jumla ya michango ya maoni 33, kutoka mabara matano.
Na kwamba, Makadinali bado wanaona haja ya kuwa na muda zaidi wa maandalizi ya kutosha kwa ajili ya vikao muhimu vya Conclave. Padre Lombardi anasema, hakuna sababu za kuharakisha.
Na pia alitangaza kwamba, mchana Jumatano , majira ya saa 11 za jioni, katika Madhabahu Kuu ya Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro , Makardinali watakusanyika kwa ajiliya Ibada ya Kuabudu na masifu ya Jioni, wakiongozwa na Decano wa Decania ya Makardinali , Kardinali Angelo Sodano. Makardinali kwametoa mwaliiko kwa kanisa zima, kuungana nao wakati huo , kwa ajii ya kuiombea kazi hii muhimu ya uchaguzi kwa Kanisa.
Aidha Padre Lombardi amesema, kwa ajili ya kazi za kuandaa kikanisa cha Sistine, kwa uchaguzi: Kikanisa hicho kimefungwa tangu leo kwa watalii na wageni.
Na hatimaye, Padre Lombardi alitoa taarifa juu ya uwepo wa vyombo vingi vya habari, vilivyofika Roma kwa ajili ya uchaguzi huu akitaja kwamba, kuna wanahabai karibia 4,432 wenye dhamana waliotoka mataifa 65 kwa ajili ya utoaji habari katika lugha mbalimbali 24.








All the contents on this site are copyrighted ©.