2013-03-04 16:17:43

Waluteri wamshukuru Papa Mstaafu Benedikto XV1


Shirikisho la Waluteri la Dunia (LWF), limetoa shukurani kwa Baba Mtakatifu Mstaafu Benedikto XV1, kwa juhudi alizoonyesha katika kujenga mshikamano na umoja wa Wakristu yaani uekumene , hasa katika siku za mwisho wa utawala wake.
LWF, katika barua yake iliyotiwa sahihi na Rais wa LWF, Askofu Munib Younan na Katibu Mkuu Martin Junge, mmeandikwa , "Tumejisikia kutiwa nguvu na ahadi yake inayothamini kwa kina majadiliano ya kiteolojia na kuekumeni , yanayolenga kuupata umoja kamili wa Kanisa hata katika misingi ya majiundo thabiti ya miito kwenye Ushariki wa Waluteri.
Viongozi hao wametoa ahadi ya kutunza waliyo jadili katika mkutano pamoja na Papa Benedikto XV1, hapo Desemba 2010, ambamo kwa namna ya kipekee, alisisitiza majiundo msingi ya pamoja kati ya waluteri na Wakatoliki,na hasa tafakari za pamoja wanapotembea katika njia ya kuelekea umoja kamii.
Barua ya LWF, inaendelea kutoa shukurani kwa Papa msaatafu, kwa jinsi alivyo liongoza Kanisa Katoliki, katika kuwa na mwendelezo wa majadiliano juu ya Uinjilishaji mpya. juhudi hizo, zimechochea pia makanisa mengine ya Kikristu kutafakari juu ya wajibu wao, katika kushiriki kwenye utume wa Mungu, kwenye dunia ya sasa.
Barua inaeleza, kwanza, walishtushwa na taarifa ya kustaafu kwa Papa , lakini baada ya kutafakari kwa kina sababu za kustaafu kwake, wameona kwamba, ni kitendo cha hekima na busara na ushupavu wa hali ya juu , kutoa maamuzi kama hayo , kwa ajili ya manufaa ya kanisa . Ni pendo wa kina wa Papa Mstaafu kwa kanisa la Kristu, imemalizia barua hiyo.








All the contents on this site are copyrighted ©.