Vurugu za kisiasa nchini Zambia za sababisha maafa!
Heri wapatanishi maana hao wataitwa wana wa Mungu ni ujumbe kutoka kwa Baraza la Makanisa
Zambia, ambalo limesikitishwa na fujo na vurugu zilizojitokeza hivi karibuni nchini
Zambia kiasi cha kupelekea baadhi ya watu kupoteza maisha yao walipokuwa wanashiriki
katika uchaguzi mdogo wa Jimbo la Livingstone.
Baraza la Makanisa Zambia lina
laani vitendo vya vurugu vinavyosababishwa na masuala ya kisiasa na wanawaomba wananchi
wa Zambia kuwa watulivu na kuachana na ushabiki unaoweza kusababisha maafa makubwa
kwa watu wasiokuwa na hatia n chini Zambia.
Jeshi la Polisi litekeleze wajibu
wake kwa kuzingatia sheria za nchi. Huu si wakati wa kutupiana lawama, bali kila upande
uchunguze dhamiri na kuangalia kiwango cha kisiasa kilichofikiwa na wananchi wa Zambia
na kuhoji ikiwa kama hii ndiyo njia sahihi wanayopaswa kuichukua!