Rais Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda pamoja na familia yake wanaomboleza kifo cha
Mzee Amos Kaguta, baba yake mzazi wa Rais Museveni aliyefariki dunia Ijumaa, tarehe
22 Februari 2013 akiwa na umri wa miaka 96. Mipango ya mazishi inaendelea kufanywa
nyumbani kwa Mzee Amos Kaguta huko Rwachitura, Magharibi mwa Uganda, yaani kilometa
mia 200 kutoka Jijini Kampala.
Familia ya Rais Museveni wa Uganda inawashukuru
madaktari wa Hospitali ya Kimataifa, Kampala waliomhudumia Mzee Amos Kaguta, hadi
pale Mwenyezi Mungu alipoamua kumwita mja wake kutoka bondeni huku kwenye machozi.
RIP.