2013-02-21 09:24:52

Caritas Sahel na mikakati ya kuwajengea wadau uwezo wa kupambana na majanga!


Shirika la Misaada la Kanisa Katoliki Ukanda wa Sahel, Caritas linaendelea na mkutano wake uliofunguliwa hapo tarehe 19 na unatarajiwa kuhitimishwa tarehe 23 Februari 2013. Wajumbe wanajadili pamoja na mambo mengine hali ya kisiasa, kijamii na baa la njaa katika Ukanda wa Sahel ili kuweza kujipanga vyema zaidi kuokoa maisha ya watu. Mkutano unawashirikisha wajumbe wa Caritas kutoka: Burkina Faso, Mali, Niger na Senegal, nchi ambazo tangu mwaka 2007 zimeandaa Jukwaa la Mikakati ya Caritas Ukanda wa Sahel.

Wajumbe wanataka kuimarisha mawasiliano katika kukabiliana na hali mazingira magumu kwa kujenga uwezo kwa Mashirika ya Caritas katika nchi husika, ili kushiriki kikamilifu katika kuwahudumia wahanga wa machafuko ya kivita nchini Mali. Hadi sasa takwimu zinaonesha kwamba, kuna jumla ya watu zaidi ya 300,000 ambao wamekimbia kutoka Mali na wanapata hifadhi katika mipaka ya nchi jirani.







All the contents on this site are copyrighted ©.