2013-02-20 16:00:02

Marehemu Padre Evarist Mushi amezikwa Zanzibar


Marehemu Padre Evarist Mushi, wa Kanisa Katoliki la Mtakatifu Joseph la mjini Magharibi Zanzibar aliyeuawa kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana Zanzibar Jumapili iliyopita, Jumatano hii amezikwa kwa heshima kubwa. Ibada ya Misa ya wafu iliyosomwa kwa nia ya kumwombea Marehemu ilifanyika katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Josef la Minara Miwili, Zanzibar.
Viongozi mbalimbali wa Kanisa na kijamii wamehudhuria mazishi haya, akiwemo Rais wa Zanzibar , Dr Al Mohamed Shein, viongozi wengine wa ngazi za juu wa vyama vya kisiasa na kijamii, na uwakilishi mkubwa kutoka viongozi mbalimbali wa makanisa mengine kama KKKT, Anglican, Pentecoste na jumuiya za kikanisa.
Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, aliongoza Ibada ya Misa ya Wafu, akisaidiana na Askofu Mkuu Paulo Ruzoka wa Jimbo Kuu la Tabora, na Askofu Tarcisio Ngararakumtwa, wa Jimbo la Iringa na Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania(TEC) . Marehemu Padre Evaristi Mushi aliuawa kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikani wakati akiwa katika harakati za kwenda kuadhimisha Misa katika kanisa lake.
Askofu Augostine Shayo, wa Jimbo la Zanzibar, akieleza kwa nini wameamua Padre Mushi aliyeuawa akiwa na umri wa miaka 55, azikwe Zanzibar badala ya kwao Moshi ameeleza kwamba, Padre Evaristi , ameishi Zanzibar tangu akiwa na umri wa miaka kumi na nane na hivyo ni mkazi wa Zanzibar, na amezikwa katika kiunga cha Kitope.
Taarifa zinabaini , katika ukweli wake, pamoja na viongozi wa serikali kukemea maovu na chuki za kidini dhidi ya Wakristu, siku tatu tu baada ya kuuawa kwa Padre Evarist Mushi, Kanisa la The Pool of Siloam la Zanzibar, lilichomwa moto na watu wasiojulkana na kuharibu i zake kuharibiwa.
Naibu Kamisheni wa Polisi , Yusuf Ilembo, amenukuliwa na vyombo vya habari, akithbitisha uwepo wa tukio hilo la kusikitisha, ambalo limeongeza maumivu katiak vidonda vingine vya uhalifu kama huo. Anasema, tukio hilo lilitokea jana majira ya saa kumi za usiku kuamkia Jumanne, katika wilaya ya kati Mkoa wa Kusini Unguja. Na Mkuu w Polisi nchini Tanzania, ametoa amewaonya wote wanaohusika na madhulumu haya kwamba , kwa hakika watawajibika kwa mujibu wa sheria za nchi.








All the contents on this site are copyrighted ©.